Swahili
Surah Al-Balad ( The City ) - Aya count 20
لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ 
( 1 ) 
Naapa kwa Mji huu!
وَأَنتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ 
( 2 ) 
Nawe unaukaa Mji huu.
وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ 
( 3 ) 
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي كَبَدٍ 
( 4 ) 
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ 
( 5 ) 
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا 
( 6 ) 
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُ أَحَدٌ 
( 7 ) 
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ 
( 8 ) 
Kwani hatukumpa macho mawili?
وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ 
( 9 ) 
Na ulimi, na midomo miwili?
وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ 
( 10 ) 
Na tukambainishia zote njia mbili?
فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ 
( 11 ) 
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ 
( 12 ) 
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
فَكُّ رَقَبَةٍ 
( 13 ) 
Kumkomboa mtumwa;
أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ 
( 14 ) 
Au kumlisha siku ya njaa
يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ 
( 15 ) 
Yatima aliye jamaa,
أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ 
( 16 ) 
Au masikini aliye vumbini.
ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ 
( 17 ) 
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ 
( 18 ) 
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ 
( 19 ) 
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌ 
( 20 ) 
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.