Swahili
Surah Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya count 30
وَالْفَجْرِ 
( 1 ) 
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍ 
( 2 ) 
Na kwa masiku kumi,
وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ 
( 3 ) 
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ 
( 4 ) 
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ 
( 5 ) 
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ 
( 6 ) 
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ 
( 7 ) 
Wa Iram, wenye majumba marefu?
الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ 
( 8 ) 
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ 
( 9 ) 
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ 
( 10 ) 
Na Firauni mwenye vigingi?
الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ 
( 11 ) 
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ 
( 12 ) 
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ 
( 13 ) 
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ 
( 14 ) 
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ 
( 15 ) 
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ 
( 16 ) 
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ 
( 17 ) 
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ 
( 18 ) 
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا 
( 19 ) 
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا 
( 20 ) 
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا 
( 21 ) 
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا 
( 22 ) 
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ 
( 23 ) 
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي 
( 24 ) 
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ 
( 25 ) 
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ 
( 26 ) 
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ 
( 27 ) 
Ewe nafsi iliyo tua!
ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً 
( 28 ) 
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَادْخُلِي فِي عِبَادِي 
( 29 ) 
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَادْخُلِي جَنَّتِي 
( 30 ) 
Na ingia katika Pepo yangu.