Swahili
Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya count 36
وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ
( 1 ) 
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
( 2 ) 
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
( 3 ) 
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
( 4 ) 
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ
( 5 ) 
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ
( 6 ) 
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ
( 7 ) 
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ
( 8 ) 
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ
( 9 ) 
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
( 10 ) 
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ
( 11 ) 
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
( 12 ) 
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
( 13 ) 
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ
( 14 ) 
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ
( 15 ) 
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ
( 16 ) 
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
( 17 ) 
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ
( 18 ) 
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ
( 19 ) 
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ
( 20 ) 
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ
( 21 ) 
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
( 22 ) 
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ
( 23 ) 
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ
( 24 ) 
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ
( 25 ) 
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ
( 26 ) 
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ
( 27 ) 
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ
( 28 ) 
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ
( 29 ) 
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
( 30 ) 
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ
( 31 ) 
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ
( 32 ) 
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ
( 33 ) 
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
( 34 ) 
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ
( 35 ) 
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ
( 36 ) 
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?